
Erick Kabendera
Kabendera amefikishwa Mahakamani hapo akiwa bado anatembea kwa kuchechemea na kuieleza mahakama hiyo kwamba, alipelekwa katika Hospitali ya Amana kwa ajili ya vipimo na majibu ya vipimo hivyo yalionesha kuwa ana matatizo hayo.
Kabendera ameyabainisha hayo mbele ya Hakimu Mkazi mwandamizi Agustine Rwizile, baada ya Wakili mwandamizi wa Serikali Wankyo Simon, kueleza shauri hilo lilifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Hata hivyo, kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 01, 2019.
Kabendera alifikishwa mahakamani hapo Agosti 5, 2019, akikabiliwa na mashtaka matatu ambayo ni kuongoza genge la uhalifu, kukwepa kodi na kutakatisha fedha zaidi ya Sh milioni 173.2.