Mkuu wa wilaya ya Nyamagana,Dkt Phillis Nyimbi
Hayo yamebainishwa jijini Mwanza na Meneja wa bima kanda ya Ziwa Sharif Hamad, kwenye hafla iliyofanywa na kampuni ya bima ya Icea Lion, ambapo makundi hayo yametakiwa kjiunga na bima ili kuepukana na kununua ama kufanya marekebisho ya mara kwa mara.
Awali akifungua hafla hiyo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella, mkuu wa wilaya ya Nyamagana Dkt Phillis Nyimbi, amesema makundi mbalimbali yakiwemo ya wafanyabiashara na wakulima yanatakiwa kupewa elimu ya namna ya kukata bima.
Kampuni ya bima ya Icea Lion, imekuwa ikitoa huduma ya bima kama bima ya ujenzi, magari, biashara, safari, usafirishaji, viwanda, vituo vya mafuta bima ya moto kwa nyumba binafsi na viwandani, bima za meli, ndege, wizi na bima nyingine.