Katika mahojiano aliyofanya Gareth Southgate, amesema ukweli ni kwamba Lingard anapitia wakati mgumu na yeye mwenyewe anajua hilo, hivyo hakuna maajabu yeye kutomuita kwenye kikosi chake.
'Lingard anajua kuwa anapitia wakati mgumu kutokanana na nafasi anayocheza ya kiungo mshambuliaji, unapimwa kwa vitu viwili tu, magoli unayofunga au msaada wa magoli unaotoa na si vinginevyo', amesema.
Southgate ameongeza kuwa kwenye kikosi chake kwa sasa kuna wachezaji wa eneo la kiungo mshambuliaji wengi na wanafanya vizuri na ni vijana pia kama Jadon Sancho, hivyo wanahitaji nafasi zaidi.
UANGALIZI WA UEFA
Kwa upande mwingine Shirikisho la soka barani Ulaya (UEFA), limeweka wazi kuwa litaweka waangalizi kwenye michezo ya baadhi ya mataifa ili kuhakikisha wanabaini na kukomesha vitendo vya ubaguzi vinavyoonekana kushamili kwenye soka la Ulaya.
Gareth Southgate explains why Jesse Lingard was left out of the @England squad. pic.twitter.com/SYEyPsCz0T
— The Sun Football (@TheSunFootball) October 10, 2019
