
Msisitizo umeedelea kuwekwa kwa Jeshi la kujenga Taifa kuongeza kasi ya ujenzi wa nyumba katika kijiji cha Msomera,ili iweze kuendana na kasi ya wanao jiandikisha.
Akitoa taarifa ya Maendeleo ya zoezi hilo kwa msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa ,naibu kamishna wa uhifadhi NCAA Dkt Christopher Timbuka amesema kwa sasa idadi ya wanao jitokeza kujiandikisha kwa hiari imekuwa maradufu na kuanza kutishia upatikanaji wa nyumba kule Msomera
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Ngorongoro Raymond Mangwala amesema hali ya uhifadhi wa mimea na wanyamapori katika maeneo waliyohama wananchi imeanza kurejea kwa kasi, kwani kwa sasaa inawezekana kuona wanyama wote wakubwa almarufu the BIG FIVE