Jumapili , 20th Jan , 2019

Baada ya Mahakama Kuu ya Kikatiba ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kumtangaza Kiongozi wa upinzani, Bw. Felix Tshisekedi kuwa mshindi wa uchaguzi wa Urais, Rais John Magufuli amempongeza Rais huyo mteule na kumuahidi kuendeleza ushirikiano.

Rais John Pombe Magufuli

Rais Magufuli ametoa pongezi hizo leo Januari 20, ambapo mbali na kumpongeza Rais Mteule amewapongeza pia raia wa Kongo akiwataka kuduisha  amani.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Magufuli ameandika, "Kufuatia hukumu ya Mahakama Kuu ya Katiba. Ninampongeza Felix Tshisekedi juu ya uchaguzi wake kama Rais wa DRC.

"Ninapongeza pia Wakongo wote, ninawasihi kudumisha amani . Ninaahidi kuendeleza uhusiano wetu wa kihistoria na wa kindugu" Rais Magufuli.

Katika uchaguzi huo uliofanyika Desemba 30 2018, Mgombea Martin Fayulu alidai kuwa ndiye mshindi wa kiti hicho cha Urais, amezitaka Jumuiya za kimataifa kutomtambua Tshisekedi, akidai kuwa yeye ndiye mshindi halali wa uchaguzi huo.