Jumatatu , 29th Mar , 2021

Wananchi wa kijiji cha Chimati kilichopo wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma wameishukuru serikali kwa kuwaletea mradi mkubwa wa maji ambao umewasaidia kuondokana na kero mbalimbali ikiwemo kuvunjika kwa baadhi ya ndoa kutokana na kufuata maji umbali mrefu.

Wananchi wa kijiji cha Chimati wakiwa na mkuu wa wilaya ya Nyasa Mh. Isabela Chilumba

Wakiongea wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huo ulio kamilika kwa asilimia 85 na kugharimu kiasi cha shilingi milioni 356, wananchi wa kijiji cha Chimati kilichopo wilaya ya Nyasa mkoa wa Ruvuma wamesema walikuwa wanapata kero kubwa ya upatikanaji wa maji safi na salama.

''Tulikuwa tunapata taabu kufuata maji mbali  hali iliyokuwa inasababisha ndoa nyingi kuvunjika. Tunaishukuru serikali kwa mradi huu ambao unaondoa kero hiyo kubwa'', amesema Amos Mbemba mkazi wa kijiji cha Chimati.

Kufuatia mradi huo kuanza kutoa maji katika kijiji hicho lakini matunzo ya mradi huo kwa wananchi yamekua mabovu hali hiyo ikamsikitisha mkuu wa wilaya ya Nyasa Mh. Isabela Chilumba na amewataka wananchi hao kutunza miradi ambayo serikali inaileta kwa ajili yao.