
Kiongozi huyo wa ngazi ya juu Bw.Saulos Chilima anatuhumiwa kupokea dola zakimarekani 280,000 amabzo ni sawa na zaidi ya shilingi milioni 654 kutoka kwa mfanyabiashara ili kusaidia kupata tenda za serikali.
Anatarajiwa kupandishwa mahakamani ambako atakabiliwa na mashtaka sita yanayohusiana na ufisadi, shirika hilo limesema.
Bw Chilima bado hajazungumzia madai hayo, lakini tovuti moja ya habari nchini humo imesambaza picha yake akiwasili mahakamani katika mji mkuu wa Lilongwe.