
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha ADC, Queen Sendiga.
Bi. Sendiga ametoa kauli hiyo leo wakati akiwahutubia wakazi wa Manzese Jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa elimu ya ufundi itasaidia kuongeza soko la ajira nchini na kuongeza wabunifu nchini.
Aidha, Sendiga ameongeza kuwa ataondoa vikwazo vilivyopo katika sekta za ajira ambapo wahitimu wengi hukosa ajira kwa kutakiwa kuwa na uzoefu, hivyo katika uongozi wake atalikomesha hilo.
“Endapo nikichaguliwa kuwa Rais wa Tanzania, nitaondoa vikwazo vyote katika soko la ajira, masuala ya kuombwa uzoefu wakati umetoka shule hayatakuwepo katika uongozi wangu”, amesema Sendiga.