Waziri wa Nchi, Sera,Bunge,Ajira,Vijana na Wenye Ulemavu,Jenista Mhagama
Wakizungumza hii leo katika mkutano na waandishi wa habari,kupitia Katibu Mtendaji Anna Ryoba Paul, wanawake viongozi wamelipongeza jeshi la polisi kwa jitihada zake za kulinda amani katika kipindi hiki cha uchaguzi.
'' Pia tunawataka viongozi wa siasa kutotumia viongozi wa dini katika siasa ili kuepusha mgawanyiko miongoni mwa wananchi ''Alisema katibu huyo Anna Paul
Naye Waziri wa Nchi, Sera,Bunge,Ajira,Vijana na Wenye Ulemavu,Jenista Mhagama, ameungana na viongozi hao kwa kuzungumza nao kwa njia ya simu katika mkutano huo na kusema kuwa hatua hiyo ni nzuri kwa nafasi walionayo na ni jukumu lao kulinda na kudumisha amani ya nchi yao.
''Kukutana kwenu kuna umuhimu katika kufanya maamuzi ya kuchagua viongozi mnaowataka na mna jukumu kubwa la kuhamasisha na kuilinda amani ya nchi.''Mh. Jenista aliongeza
Aidha Mh. Jenista amesema kuwa waathirika wakubwa iwapo amani na utulivu vitatoweka ni wanawake na kuwaasa watu wote kuwa kuna maisha baada ya uchaguzi hivyo ni muhimu kuilinda amani ya nchi na siku ya kupiga kura wajitokeze kwa wingi.