Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Christine Mndeme
Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 13, 2021, kwenye kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio na kusisitiza kuwa wanawake wanapaswa kujiamini kwani kila analoliweza mwanaume na mwanamke analiweza.
"Nilipokuwa Mkuu wa wilaya fulani kulitokea mapigano makubwa ya wakulima na wafugaji nilienda mwanamke mwenyewe katikati ya wanaume wakiwa na silaha kali za kijadi na nilitatua ule mgogoro na niliwauliza mbona mko wanaume tu, wakanijibu wanawake wapo nyumbani sisi ndiyo tunapambana," amesema Mndeme.