Ijumaa , 21st Oct , 2022

Wabunge wa conservative wanaotarajia kumrithi Liz Truss kama waziri mkuu wapo mbioni kutafuta ushawishi kutoka kwa wabunge wa chama kabla ya tarehe ya mwisho ya Jumatatu wiki ijayo.

 

Bi Truss alijiuzulu siku ya jana ikiwa ni  wiki sita tu katika toka aanze kazi hiyo, na kufanya uwaziri wake wenye misukosuko kuwa mfupi zaidi katika historia ya Uingereza.

Wagombea wanaotaka  kuchukua nafasi yake wanahitaji uungwaji mkono kutoka kwa wafuasi wa Liz wasiopungua 100, na kupunguza ushindani hadi watatu.

Waziri Mkuu wa zamani Boris Johnson hajaondoa uwezekano wa kugombea tena ikiwa ni  miezi kadhaa baada ya kulazimishwa kuondoka baada ya uasi wa Tory.

Wengineo Rishi Sunak na Penny Mordaunt, ambao walisimama bila mafanikio katika kinyang'anyiro cha kuchukua nafasi yake, pia wanaonekana kuwa washindani wa kugombea tena