Alhamisi , 3rd Nov , 2016

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri amewaagiza viongozi na watendaji wote mkoani humo kusimamia mpango maalum wa ushirikishwaji kati ya walimu na wanafunzi ili kusaidia kuinua kiwango cha elimu katika mkoa wa Tabora.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mh. Aggrey Mwanri, akitoa somo la fursa kwa baadhi ya wananchi wake

 

Akizungumza katika mafunzo maalum ya waratibu elimu kata wa mkoa huo wilayani Urambo Mwanri amesema tangu mpango huo ulipoanza utekelezaji wake mwaka 2015 umeanza kusaidia mkoa hadi kushika nafasi ya 10 kitaifa mwaka huu kutoka nafasi ya mwisho kwa miaka minne mfululizo.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema usimamizi mbovu wa watoto hapo awali ulikua unawafanya watoto wengi kutumikishwa katika kazi mbalimbali mkoani humo hali iliyokuwa inafanya washindwe kuzingatia masomo na wengine kuacha kabisa shule.

Mwanri amesema kuwa mkoa wa Tabora watoto wengi wanatumikishwa kwenye mshamba ya tumbaku,mashamba ya mpunga pamoja na migodi hivyo amewataka wazazi wawe na mahusiano mazuri na walimu ili kuboresha sekta ya elimu katika mkoa huo.