Jumatano , 21st Aug , 2019

MwanaHipHop kutokea kundi la Weusi Nikki Wa Pili, ameeleza sababu ya watu maarufu kupenda kujibu maoni 'Comments' za watu maarufu wenzao, kupitia mitandao ya kijamii, tofauti na watu wa kawaida.

Nikki Wa Pili ameeleza hayo baada ya kuandika katika mtandao wa kijamii wa Twitter  kuwa

Nimewahi kuona watu wakishambulia watu maarufu mitandaoni, kuwa wanajibu comment za watu maarufu wenzao, kiukweli bora wajibu hizo sababu inakua ni maongezi yenye staha, watu wengine hawana ustaarabu au wanatafuta vijisifa au hawajui kutawala, hisia zao yaani nivichekesho

Baada ya kuandika hivyo kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter Nikki Wa Pili alishambuliwa na watu kwa maneno kwa lugha chafu huku wakisema,

"Si sawa kwa watu maarufu kufanya hivyo, kwa sababu wakitaka kusaidiwa wanawaomba watu wa kawaida na sio watu maarufu wenzao, kwa pia watu wa kawaida wapo wengi kuliko watu maarufu” aliandika moja ya watu ambao ni wanamfuatilia kwenye ukurasa wake.

Msanii huyo kwa sasa hivi amekuwa akijiachia zaidi katika mitandao ya kijamii, akimuonesha mpenzi wake Miss Joan 'Mama Zuri'.