Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge
Amesema hayo leo Julai 25, 2020 hii wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofika uwanja wa taifa kuuangalia hatua zinazoendelea ambapo amesema wamejipanga vizuri katika kuhakikisha usalama kwa raia unakuwepo.
“Nataka kuwahakikishia wananchi wa mkoa wa Dar es salaam hali ya usalama ni nzuri, na tumejipanga vizuri, vyombo vyetu vimekaa vizuri kwahiyo tusiwe na wasiwasi tujitokeze kwa wingi nakuaga kutakuwa kuanzia asubuhi hadi jioni”.
Aidha Mkuu wa mkoa huyo amewaomba wale ambao hawatapata nafasi yakuingia uwanjani siku ya kesho wawepo barabarani mara watakapopatiwa ratiba juu ya njia watayopitia ili waweze kumuaga kutokana na sehemu waliokuwepo.