
NWS myiasis ni vimelea vinavyovamia vyenye mabuu ya inzi, au funza, wenye kusababishwa na inzi.
Wadudu hao kimsingi huathiri mifugo, na mamlaka zinasema kuwa hatari kwa afya ya umma Marekani kwa sasa "iko chini sana".
Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) vilishirikiana na idara ya afya ya Maryland kuchunguza kisa hicho.
Vimelea hao waharibifu, ambao hula tishu hai, mara nyingi hupatikana Amerika Kusini na Caribbean.
Licha ya juhudi za kukomesha kuenea kwake kaskazini, sasa visa vya ugonjwa huo vimethibitishwa katika kila nchi ya Amerika ya Kati, pamoja na Mexico.
Binadamu, haswa wale walio na jeraha la wazi, wanaweza kushambuliwa na vimelea hivyo na wako katika hatari kubwa zaidi kama watasafiri kwenda katika maeneo hayo au kama wako karibu na mifugo katika maeneo ya vijijini ambako kuna inzi, CDC inasema.