Jumatatu , 23rd Aug , 2021

Wafanyakazi watano wa TRA wamefariki dunia kwa ajali ya gari mkoani Songwe alfajiri ya leo baada ya gari lao kuligonga lori aina ya Fuso kwa nyuma, wakati wakifukuzana na gari iliyodhaniwa kubeba magendo.

Eneo la ajali iliyouwa wafanyakazi wa TRA

Akizungumza hii leo Agosti 23, 2021, na EATV & East Africa Radio Digital, Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe ACP Janeth Magomi, amesema kwamba ajali hiyo imetokea majira ya saa 11:45 alfajiri katika eneo la Hanseketwa- Old Vwawa.

Kamanda Magomi amesema kwamba ajali hiyo imesababisha vifo vya wafanyakazi wanne wa TRA mkoa wa Mbeya na mmoja wa TRA Tunduma, ambapo wote walikuwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya doria mipakani kwa lengo la kukomesha biashara ya magendo.

Miili ya marehemu hao wote imehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Songwe.