Jumatatu , 24th Oct , 2022

Rais wa Kenya Dr. William Ruto, amesema yupo tayari kufanya kazi na mmoja wa vigogo wa muungano wa Azimio Kalonzo Musyoka.

Ruto amesema amekuwa akimtafuta kiongozi huyo wa chama cha Wiper ili ampe majukumu ya kiserikali
“Nipo tayari kufanya kazi na Kalonzo wakati wowote ule, atakapokuwa tayari,” amesema Ruto. 

Musyoka alikuwa makamu wa rais wakati wa utawala wa hayati Mwai Kibaki na amewahi kuwa waziri wa mazingira, mambo ya nje na elimu chini ya utawala wa hayati Daniel Arap Moi