
Jaji Martha Koome wa mahakama hiyo akisoma hukumu hiyo amesema hakuna ushahidi wa moja kuwa moja unaoweza kubatilisha matokeo ya uchaguzi huo
Mahakama hiyo imesema hakuna ushahidi unaoonesha kwamba mfumo wa kuhesabu matokeo nchini humo uliingiliwa na mahakama haijashawishika kwamba viwango vya teknolojia ya IEBC vilifeli na kwamba fomu zilizohitajika 32A zilijazwa kwa mafanikio
Aidha hakuna ushahidi wowote kwamba Tume ya uchaguzi ilifanya makusudi kuahirisha uchaguzi katika baadhi ya maeneo ili kumkandamiza Raila Odinga
Upande wa Raila Odinga uliwasilisha hoja tisa za kupinga matokeo ya uchaguzi huo na mahakama imesema nyingi zilikuwa hazina ukweli