Jumamosi , 13th Aug , 2022

Mgombea Urais nchini Kenya kupitia muungano wa Kenya kwanza William Samoei Ruto, amewapongeza washindi wote walioshinda katika maeneo mbalimbali nchini humo

 

Ruto ametumia mtandao wake wa Twitter kuwapongeza washindi mbalibali wakiwemo wabunge hasa akieleza kufurahishwa na muamko wa wanawake katika uchaguzi huo

"Hongera kwa washindi wote wa uchaguzi. Hasa, tunasherehekea wanawake wengi ambao wamevunja vizuizi vya kupanda ngazi ya kisiasa. Kila la heri unapoanza majukumu yako mapya. Hustlers wanakutegemea" ameandika katika mtandao wake wa Twitter