Jumapili , 31st Jul , 2022

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, amemuambia  William Ruto, kwamba hana haja ya kuwaambia watu kuwa anataka kumuua na kusema yeye amekuwa akimtukana Kenyatta kwa takribani miaka mitatu na hajawahi kumgusa na kumtaka auze sera zake na aachane naye.

Kushoto ni Rais Uhuru Kenyatta, na kulia William Ruto

Kauli hiyo ameitoa hii leo Julai 31, 2022, wakati akifungua rasmi matumizi ya barabara za juu za Nairobi Expressway.

"Hakuna haja ya kuwaambia watu nataka kukuua, mmenitusi karibu miaka mitatu, kuna mtu amewagusa, si nilikuwa na uwezo, sasa sina uwezo ndiyo niko na time ya kukutafuta, piga story uza sera yako achana na mimi, mimi nafanya kazi yangu nimalize, nyie ombeni kura wananchi wakiwapatia sawa, wakiwanyima twende nyumbani pamoja, shida iko wapi si dunia itaendelea," amesema Rais Kenyatta.