Jumatano , 14th Jul , 2021

Mkuu wa mkoa wa Geita Rosemary Senyamule, ameagiza wanafunzi 11 wa shule ya Sekondari Geita wafukuzwe shule na wengine 24 wasimamishwe masomo kwa siku 30, kufuatia matukio matatu ya moto yaliyoikumba shule hiyo ndani ya mwezi mmoja uliounguza mabweni pamoja na jengo la maabara na vifaa.

Mkuu wa mkoa wa Geita Rosemary Senyamule

Hatua hiyo imekuja baada ya usiku wa kuamkia leo Julai 14 mwaka huu, moto mwingine kuzuka na kuteketeza bweni la wavulana, ambapo pamoja na hatua hizo pia ameagiza walimu 13 wachukuliwe hatua za kinidhamu ikiwemo kuhamishwa. 

Mbali na hayo shule hiyo pia imefungwa kwa wiki mbili kwa ajili ya ukarabati ili wanafunzi watakaporudi wakute miundombinu yake imerejea katika hali ya kawaida.