Pichani ni Nabii namba saba aliyetangaza anatibu virusi vya Corona, na Waziri wa Afya Dkt Faustine Ndugulile
Dkt Ndugulile amesema kuwa endapo watabaini mtu huyo hana utaalamu katika kile alichokitangaza, Serikali itamchukulia hatua stahiki na kuwataka wananchi kuepuka kutoa kauli ambazo zitachanganya jamii.
"Sisi tumeona hizo clip ambazo zinazunguka na sisi tumetuma timu yetu ya wataalam ili huyo bwana akatuthibitishie kama ana uwezo wa kufanya tiba hiyo na atuambie hiyo dawa yake imesajiliwa wapi na yeye amesajiliwa wapi na lini" amesema Dkt Ndugulile.
Hivi karibuni zilisambaa video mbalimbali katika mitandao ya kijamii, zikimuonesha Mosses Mollel, maarufu kama Nabii namba saba, kwamba anao uwezo wa kutibu virusi vya Corona.