Mkuu wa wilaya ya Rorya Juma Chikoka
DC Chikoka ametoa kauli hiyo alipotembelea soko hilo na kukuta hakuna huduma ya choo kwa takribani miaka kumi na soko hilo lipo pembezoni mwa Ziwa Victoria.
Wafanyabiashara wa soko hilo wamedai kwamba kukosekana kwa choo hicho kunaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa kwa kuwa wako karibu na Ziwa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Mkengwa Mauna Iddy, amesema kuwa wataalaamu wa Halmshauri walishafika kijijini hapo na kukutana na serikali ya Kijiji kwa ajili ya kutatua changamoto hiyo lakini mpaka sasa hakuna huduma ya choo licha ya kukusanya mapato zaidi ya shilingi milioni 10 kila mwezi kutoka katika soko hilo.
