Alhamisi , 26th Aug , 2021

Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, imeomba kibali kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai, kwa ajili ya kukamatwa kwa mbunge wa Ukonga Jerry Silaa kwa kosa la kudharau wito wa kamati hiyo leo Agosti 26, 2021, baada ya kuhojiwa kwa mara ya kwanza Agosti 24 na kutakiwa kurudi leo.

Kushoto ni Spika wa Bunge Job Ndugai na kulia Mbunge wa Ukonga Jerry Silaa.

Kibali hicho kimeombwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Emmanuel Mwakasaka, na kwamba kibali hicho kitakapotolewa itabidi Mbunge huyo akamatwe na kufikishwa mbele ya kamati kesho Agosti 27, 2021, majira ya  saa 4:00 asubuhi.

Mbunge hiyo aliitwa mbele ya kamati hiyo kwa ajili ya kujibu tuhuma mbalimbali yakiwemo makosa ya kusema uongo na kushusha heshima na hadhi ya Bunge na atakapofikishwa mbele ya kamati na Polisi atakabiliwa na kosa la kuidharau kamati.