Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Joseph Konyo
Akielezea tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Joseph Konyo, amesema taarifa zilizosambazwa mitandoni ni za uongo, na kusema kwamba kilichofanyika ni vijana wenye nia ovu kwenda kupanga magogo katika milango ya kanisa hali iliyozua taharuki kwa wananchi
Aidha, Kamanda Konyo ameeleza kwamba Padri alikataa kuendesha ibada ya mazishi ya marehemu huyo kwa madai ya kwamba marehemu alikuwa akiishi unyumba na mume wa mtu.