
Makinda amesema hayo wakati alipokuwa akipokea taarifa ya utekelezaji wa zoezi la Sensa ya watu na makazi ambalo lilifanyika Agosti 23 mwaka huu ambapo amebainisha kufanikiwa kwa zoezi hilo zaidi ya asilimia 90 kote nchini.
Awali akieleza namna sensa ilivyofanyika kwa mkoa wa Tanga mratibu wa mkoa huo Tony Mwanjota amesema kuwa wameweza kufanikiwa kuhesabu kaya kwa asilimia 95 na kuyafikia majengo yote, kuwezesha kutoa elimu na hamasa kwa wananchi ambayo imepelekea ushirikiano mkubwa uliochangiwa na viongozi wa serikali dini na siasa
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Tanga Omari Mgumba ameeleza kuwa wanaendelea kutekeleza maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kutenga maeneo maalumu kwaajili ya kilimo ili kutumia sekta ya Kilimo katika kuwakwamua wananchi na umasikini na kuwa na chakula toshelevu wakati wote ili kuweza kuchangia pato la taifa.
Katika sensa ya watu ya mwaka 2022 mkoa wa Tanga ulikadiria kuhesabiw jumla ya Kaya 649,591 lakini ni kaya 617,431 pekee zilizohesabiwa na kufanya kufikia asilimia 95 huku sensa ya majengo ikifanikiwa kwa asilimia mia moja na hatimaye kuhesabu nyumba zipatazo 730,934.