
Akiongea na waandiashi wa habari ofisini kwake Kaimu Mtendaji Mkuu wa TEMESA Mhandisi Manase Olekujam amesema kuwa kivuko hiko kimeonekana kuwa na kutu katika baadhi ya maeneo na kutoboka baadhi ya vyuma hivyo wameamua kukifanyia ukarabati wa kina kisije leta madhara hapo baadae.
Aidha amesema kwa sasa wakati kivuko hicho kinafanyiwa matengenezo serikali imekodisha kivuko kingine kitakachokuwa kinabeba abiria pekee ili kiweze kusaidiana na kivuko kilichopo cha mv Kigamboni lakini kwa wanaotumia magari binafsi wameshauriwa kutumia daraja la Mwl Nyerere mpaka pale kivuko kitakapotengemaa.