Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump
Trump alishitakiwa na wanafunzi wa zamani waliosoma katika chuo hicho ambao walidai kutapeliwa na chuo hicho.Mwanasheria Mkuu wa New York Eric Schneiderman amesema kulipwa kwa fidia hakukutarajiwa kufanywa na Trump na ni ushindi mkubwa kwa wahanga wa chuo hicho.
Trump alifunguliwa mashitaka ya madai na wanafunzi hao kwa tuhuma za kuwapotosha na kushindwa kutimiza ahadi zilizotolewa na chuo hicho huko California na New York.
