
Kushoto ni mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella na kulia ni Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu
Waziri Ummy ameyasema hayo na kuelekeza kwamba serikali haitaweza kumvumilia kiongozi yeyote wa wilaya au mkoa ambaye hatokuwa na uwezo wa kushirikisha na kushirikiana na wenzake.
"Wakuu wa mikoa mingine wanatakiwa kujitafakari sababu hata tukikaa Bungeni tunawashangaa wabunge wenzetu wanavyogombana na wakuu wao wa mikoa, tunawaambia mbona sisi Tanga tupo vizuri na mkuu wetu wa mkoa? tena anatusemea, anatushirikisha na tunapanga naye", amesema Waziri Ummy
Aidha ameongeza kuwa, "Tanga tuna mkuu wa mkoa mzuri ambaye tunafanya kazi kama timu moja, hivyo wakuu wa mikoa wajue ukishakua kwenye nafasi hiyo maana yake ni kuwashirikisha wenzako na kushirikiana nao, kuwaongoza na kuwarekebisha wenzako"