
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wakili Amoni Mpanju
Wakili Mpanju ametoa wito huo wakati akifunga mkutano wa mwaka wa tathmini wa viongozi wa Vyuo na Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo uliofanyika kwa siku sita jijini Dodoma kuanzia Oktoba 17 hadi 22, 2022.
Akifunga Mkutano huo Mpanju amevitaka Vyuo na taasisi hizo kuweka kipaumbele katika dhana tatu za uwanagenzi, maarifa na ushirikishwaji wa jamii sambamba na kufanya tafiti huku akiwasisitiza kuzingatia sheria, taratibu na miongozo kwa miradi inayotekelezwa.
Aidha Mpanju amevitaka vyuo na taassisi hizo kuongeza nguvu katika maeneo yenye changamoto ambayo ni eneo la utafiti na huduma shirikishi na kama tatizo ni bajeti itengewe kwa mwaka wa fedha ujao wawe na ushirikiano na vyuo vya ndani na nje ya nchi.