Jumamosi , 4th Mar , 2023

Wakili Richard Alex Murdauph (54) wakili na  raia wa Carolina Kusini, ahukumiwa kifungo cha maisha siku ya Ijumaa kwa kumuua mkewe na mwanawe katika kile waendesha mashtaka walisema ni jaribio la kuficha uraibu wake wa dawa za kulevya na wizi wa mamilioni ya dola

Jaji wa Mahakama ya Mzunguko Clifton Newman amemhukumu Murdaugh kifungo kwa maisha yake yote, na masharti ya mauaji yote mawili yataendeshwa mfululizo ikiwa ni hukumu iliyoombwa na waendesha mashtaka, ambao hawakutafuta hukumu ya kifo.

Wakili huyo alikutwa na hatia mnamo Alhamisi kwa makosa mawili ya kumpiga risasi mkewe Maggie (52) na mwanawe mdogo, Paul(22) kwenye mali ya familia yao mnamo Juni 7, 2021.