Ijumaa , 21st Oct , 2022

Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 300, kwa ajili ya kujenga daraja la mto Mwandoya jimbo la Kisesa, Meatu mkoani Simiyu, ili kunusuru wananchi kusombwa na maji ikiwamo wanawake kujifungulia chini ya mti, kutokana na kushindwa kupita kwenye mto unapokuwa umejaa maji.

Daraja la mto Mwandoya

Akizungumza na wananchi baada ya kukagua ujenzi wa daraja hilo unaotekelezwa na kampuni ya mzawa wa Tanzania ANDIC LTD, Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina, amesema mbali na daraja hilo kunusuru maisha ya watu, lakini pia ni kiungo muhimu katika kukuza uchumi wa wanananchi.

"Namshukuru sana Rais Samia kwa kuridhia hilo (utoaji fedha za dharura kujenga daraja Mto Mwandoya) ndiyo maana tukaletewa hili daraja na kulijenga na kulimaliza, daraja la milioni 304, na leo tunaambiwa ndani ya mwezi mmoja maana yake mvua zinaanza sisi tuna daraja la kupita juu," amesema Mbunge Luhaga