Wakielezea tukio hilo manusura na mashuhuda wa ajari hiyo wamesema majira ya saa tisa usiku wa kuamkia leo wakati mvua ikiendelea kunyesha ghafla ilipiga radi na umeme ukakatika na baada ya kurejea walianza kusikia harufu ya vitu vikiungua
Akizungumza kwa niaba ya kamanda wa jeshi la zima moto na ukoaji Ramadhan Sebombo amesema walifanikiwa kuzima moto huo ingawa baadhi ya vyumba na mali zake zimeungua huku akisisitiza wananchi kutoa taarifa haraka yanapotoea matukio kama hayo ili kunusuru mali zao







