Jumamosi , 3rd Sep , 2022

Basi la Kampuni ya Super Najmunisa lililokuwa likitoka Jijini Dar es salaam kuelekea Mkoani Mwanza limegongana uso kwa uso na Fuso katika eneo la Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi 56.

Picha ya ajali ya basi la abiria lililogongana na fuso eneo la Ibadakuli Shinyanga

Kaimu Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoa wa Shinyanga Leonard Nyandahu amesema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva la basi kutofuata sheria za barabarani na kuendesha kwa mwendo kasi na kusababisha ajali hiyo eneo la Ibadakuli Shinyanga.

Aidha Kamanda Nyandahu amesema ajali hiyo imehusisha basi  la Kampuni ya Super Najmunisa yenye namba za usajili T.413 DAY likitokea Dar es salaam kuelekea Jijini Mwanza, na Fuso yenye namba za usajili T.123 DJH likitokea Mwanza kwenda Dar es salaam likiwa limebeba mzigo wa dagaa.