Jumatatu , 10th Oct , 2022

Katika kuunga mkono juhudi za serikali za kupunguza vifo vya mama na mtoto, Zahanati ya Kirumba iliyopo jijini Mwanza inayohudumia wakazi Zaidi ya elfu arobaini wa kata za Kitangiri, Kirumba Pamoja na maeneo Jirani imepokea msaada wa vifaa tiba.

Vifaa tiba vilivyotolewa ni pamoja na dawa, mashuka na vifaa vya usafi vimetolewa na Chuo Cha Usimamizi wa Fedha IFM Kampasi ya Mwanza ili kutimiza azma ya serikali ya kupunguza vifo vya mama wajawazito na Watoto wachanga ambapo katika Zahanati hiyo ya Kirumba kinamama hamsini hadi sitini hujifungua kila mwezi

Kwa upande wake Dkt Eusebi John ambae ni Kaimu Meneja wa Chuo Cha IFM Mwanza amesema chuo hicho kimekuwa kikifanya  shughuli mbalimbali za kijami.