Jumanne , 30th Mei , 2017

Hit maker wa ngoma ya 'Samaki' Galatone amemwaga mapovu kwa kudai wasawengi wakubwa wenye majina yao wanabebwa na kiki wala siyo mziki mzuri kitu ambacho kinawapa mashabiki tabu ya kujua uwezo wa msanii

Kwenye Story tatu ya Planet Bongo, East Africa Radio Galatone amefunguka hayo kwa kudai kwamba kiki zimewafanya wasanii wengi kuwa na majina makubwa huku kazi zao zikiwa ni mbovu kitu ambacho amekitafsiri ni kuchanganya mashabiki

Hata hivyo Galatone ameongeza kwamba jambo ambalo linaweza kuwamaliza wasanii wanaotegemea kiki ni kurudishwa kwa muziki wa bendi utakao lazimisha wasanii kuimba kwa kutumia vyombo na siyo kubebwa na kiki ambazo zinaua muziki wa bongo.

Msikilize hapa chini Galatone akifunguka.