Jumatatu , 29th Mei , 2017

Mkongwe wa bongo fleva Dully Sykes 'Mr Misifa' na  hitmaker ‘Yono’ amefunguka sababu kubwa ya kufungua studio ni kuepuka usumbufu wa kurekodi pale anapokuwa amepata mzuka pamoja na uhuru wa kujifanyia kazi zake kama msanii kwa muda wowote.

Dully Sykes

Dully amefunguka hayo hivi karibuni na kudai kuwa wasanii wanapata pesa lakini wengi wao wanaendekeza starehe sana na kusahau uwekezaji kitu ambacho yeye aliepukana nacho kwa kuhofia kupata kero kwenye shughuli zake binafsi.

“Nilifikiria nikaona kwamba nafanya muziki, kama napata idea siwezi kwenda kumgongea mtu nikamwambia kwamba naomba kurecord wakati mtu kajipumzika No! kama nina studio yangu naweza kurecord mwenyewe. Sisi wasanii tunapata hela, wasanii wanapenda starehe tu. Kwahiyo Equipments ni vitu ambavyo unaweza kununua kama ukiwa na akili hata kwa hela ndogo unayoipata” - amesema Dully.

Hata hivyo Dully ameongeza kuwa baada ya kupiga hatua mpaka kumiliki bendi na vifaa vya studio vyenye viwango ameona ni vyema kuanzisha record lebo hatua ambayo ameitaja kama moja mafanikio ya muziki wake kwa kipindi chote cha kufanya muziki.