
Msanii Foby kushoto kulia ni Ebitoke
Akipiga story na Planet Bongo ya East Africa Radio, Foby anasema sababu za kumuweka Ebitoke kwenye 'Profile' yake ni kumuelewa na kumkubali mshekeshaji huyo.
"Nampenda muda mrefu sana, napenda uigizaji wake kuna vitu fulani ananikumbusha nikiwa mtoto ili uchekeshe lazima ujipake vitu usoni hivyo napenda kitu anachofanya ndio nikaamua nimuweke profile sidhani hata kama yeye anajua" amesema Foby
Aidha Ebitoke naye alishawahi kuweka hisia zake kwa msanii Ben Pol na sasa hivi anaonyesha kumkubali zaidi msanii Alikiba.