Ijumaa , 13th Mar , 2015

Staa wa muziki wa kizazi kipya Gozby, amejipanga kuleta mapinduzi katika biashara ya muziki kwa kuuza mixtape yake kwa bei kubwa kwa malengo ya kutengeneza thamani ya kazi yake na kuzuia usambaaji wa kazi hiyo ovyo.

msanii wa miondoko ya bongofleva nchini Gozby

Gozby amesema kuwa, kupandisha bei ya kazi yake hiyo kutamfanya mnunuzi kusikia uchungu wa kumpatia mtu mwingine bure, na vilevile hatua hiyo ameichukua maalum kwaajili ya kufidia gharama kubwa alizotumia kuitengeneza.