Jumatano , 11th Jun , 2025

Msanii Ibraah amenyoosha maelezo kuhusu story zake za kuhamia katika label ya Wcb Wasafi iliyo chini ya msanii Diamond Platnumz , Chinga ameeleza hayo alipokuwa akipiga story na waandishi wa habari nchini Kenya

Pichani Ibraah na Diamond

"Kama kuna chochote kinaendelea basi mtakiona kwasababu hakuna kitakachojificha kwasababu ni kazi na tunapofanya kazi siku zote tunahitaji umoja kwahiyo kama itatokea mtaona hatutoficha chochote'' Amesema Ibraah

"Siwezi kuficha chochote kama Wcb Wasafi ndio sehemu nitakayoenda mtaona kwasababu ndio nitakuwa nafanya nao kazi lakini kwasasa tupo Oya Gang" Amesema Ibraah

 

Ikumbukwe kuwa Msanii Ibraah ameachana na label yake ya zamani Konde Gang siku za hivi karibuni na kutambulisha uongozi wake mpya ambao unaitwa Oya Gang