Jumamosi , 20th Jan , 2024

Rapa Ja Rule ametaka kupewa heshima yake aliyoitengeneza kwenye muziki wa HipHop baada ya jina lake kukosekana kwenye Listi ya Rapa 50 bora wa muda wote kupitia Billboard.

Picha ya Ja Rule

Rapa huyo amezungumza hilo juu ya kutemwa kwake kwenye orodha ya Rappers 50 bora zaidi wa wakati wote wa Billboard baada ya kuonekana kwenye ‘The Tamron Hall Show’ siku ya Alhamisi.

Katika Listi hiyo yapo majina ya rapa wengine kama Rick Ross Jadakiss, Queen Latifah, Dr Dre, Ludacris, Future, Busta Rhymes, T.I, Lil Kim, DMX, Missy Elliott, Ice Cube, 50 Cent, J Cole, Kanye West, Nick Minaj, Snoop Dogg, Drake, Lil Wayne, BIG Notorius, Eminem, Tupac Shakur, Nas, Kendrick Lamar na Jay Z.