Jumatatu , 5th Feb , 2024

Ni Headlines za mwanamuziki tajiri duniani Jay Z ‘HOV’ akiwachana waandaji wa tuzo za Grammy kutompa tuzo yoyote mke wake Beyonce kipengele cha Album bora ya mwaka.

Picha ya Jay Z usiku wa tuzo za Grammy

Jay Z amefunguka hilo wakati anapokea tuzo ya ‘Dr Dre Global Impact Award’ akihoji kuwa Beyonce ana tuzo nyingi za Grammy kuliko mtu yeyote na nyimbo zake kutoka kwenye Album ndio zinachukua tuzo kwa nini hapewi tuzo ya Album bora ya mwaka.

“Inakuaje ana tuzo nyingi za Grammy kuliko mtu yeyote, halafu unakosa tuzo ya Album bora ya mwaka? Hiyo haifanyi kazi fikirieni kuhusu hilo, wengi wataenda nyumbani kuhisi kama ameibiwa” amesema Jay Z