Alhamisi , 25th Jan , 2024

WWE Superstar John Cena amepanga kustaafu kucheza mieleka kabla ya kufikisha miaka 50 ambapo mwaka huu anatimiza miaka 47.

Picha ya mwanamieleka John Cena

Mwanamieleka huyo na muigizaji anasema kwa sasa anajisikia vizuri lakini kuwa mieleka inachukua muda wake mwingi wa usiku kupambana ulingoni.

“Naenda kutimiza miaka 47 mwaka huu, najihisi vizuri lakini kuwa mwanamieleka inakuchukua usiku na usiku kupambana”.

“Nina shauku sawa na mashabiki na ninataka kuwapa kile wanachonipa. Maili kwenye odometer husema, hilo lazima lifanyike kabla ya 50” amesema John Cena

John Cena ana rekodi ya kuwa bingwa wa dunia wa WWE mara 16 pia anatajwa kama mmoja ya wanamieleka wakubwa wa muda wote.