Ijumaa , 10th Dec , 2021

Mwanamziki Kanye West anapigiwa chapuo kurithi nafasi ya marehemu Virgil Abloh ya kuwa mbunifu mkuu wa mavazi ya kiume katika kampuni ya mavazi ya Louis Vuitton.

Picha ya Kanye West na Virgil Abloh

Kanye na Abloh walikuwa marafiki na walikutana kwa mara ya kwanza na kufanya kazi pamoja mwaka 2009 katika kampuni ya mavazi ya Fendi ya nchini Italia.

Gazeti la The Sun la nchini Uingereza limemtaja Kanye West kama mtu anaeongozwa kwa kupigiwa chapuo katika kampuni ya Louis Vuitton kwa ajili ya kuchukua mikoba ya Abloh aliyefariki kwa ugonjwa wa saratani Novemba 28 mwaka huu.