
Kushoto ni Lady Jay Dee na kulia ni msosi ambao leo umesindikiza sikukuu yake.
Kupitia mtandao wa Twitter mkali huyo wa 'Vocals' amewaambia watu ambao leo wapo sana mtandaoni huenda kwao hakuna sikukuu hivyo yeye anajiweka sawa na akishiba ndio atakuja mtandaoni kwa kasi.
''Watu wanaoshinda sana leo Twitter ujue kwao hakujapikwa na hakuna sikukuu. Mimi leo na Tweet kwa nadra, nikishiba ndio nitakuja kwa kasi jioni'', ameandika.
Watu wanaoshinda sana leo Twitter ujue kwao hakujapikwa na hakuna sikukuu. Mimi leo na tweet kwa nadra, nikishiba ndio nitakuja kwa kasi jioni
— Lady JayDee (@JideJaydee) December 25, 2018
Hata hivyo baadhi ya mashabiki wameendelea kutaniana na Lady Jay Dee wengine wakimwambia kuwa wanaoshinda mtandaoni hawajui kupika jambo ambalo limemfanya Jide aweke picha ya msosi ambao amekula.
Karibu kipenzi pic.twitter.com/AHCIEHJ1Gf
— Lady JayDee (@JideJaydee) December 25, 2018