Jumatatu , 29th Jun , 2015

Msanii wa kike kutoka nchini Tanzania Linah ameamua kujiongeza na kuanza kufanya biashara ili kujiingizia kipato zaidi nje ya muziki ambapo sasa ameamua kuwa mfugaji wa kware, baada ya kugundua uhitaji mkubwa wa mayai ya ndege hao.

Linah Sanga

Linah amesema ameamua kujiingiza katika biashara ya ufugaji baada ya kushauriwa na mama yake ambaye pia ni mshirika mwenzake kibiashara, lakini pia ili kuweza kujikimu kimaisha zaidi kwa kujiingizia kipato nje ya muziki.

Msanii huyo anaetamba na wimbo wa Hellow aliomshirikisha Cristian bella amesema kwa muda mfupi alioanza biashara hiyo imeanza kumuonesha mafanikio kwa kiasi Kikubwa.