Msanii Hussein Machozi
Hussein Machozi amesikitishwa na taarifa hizo ambapo amesema yeye ni mzima wa afya, yupo salama na kama kuna kosa alilowahi kufanya basi awaombe watu msamaha ili mradi wasimzushie taarifa hizo tena.
Kupitia akaunti yake ya mtandao wa Instagram Hussein Machozi ameeleza kuwa,
"Kah jamani mbona mnaniua namna hii, hata kama hamnipendi sio hivi asee mimi nipo salama tena nina afya tele, msinifanyie hivi jamani kwani niliwakoseaga nini mniambie basi niwaombe msamaha maana mara ya pili sasa mnaniua, ama mnataka nidedi kweli" ameandika Hussein Machoz