Meneja wa msanii Harmonize Dr Sebastian Ndege
Akizungumza kwenye Show ya SalamaNa inayoruka kila siku ya Alhamisi saa 3:00 usiku kupitia East Africa TV, Sebastian Ndege amesema kuna hisia tatu ambazo watu walikuwa na mashaka naye wakati anamchukua Harmonize.
"Kuna hisia tatu ambazo watu walikuwa wana mashaka mimi kuwa meneja wa Harmonize, moja ni kumfelisha dogo, mbili ni kumpoteza tatu ni kumtoa WCB, lakini ukweli ni kwamba mimi nilisubiri muda wake uishe ili niweze kufanya naye kazi" amesema Meneja wa Harmonize Dr Sebastian Ndege