Ijumaa , 31st Jul , 2020

Meneja wa msanii Harmonize Dr Sebastian Ndege maarufu kama Jembe ni Jembe, amesema alikuwa anatuhumiwa na watu suala la kumchukua Harmonize kwenye menejimenti aliyokuwa ili aweze kufanya naye biashara.

Meneja wa msanii Harmonize Dr Sebastian Ndege

Akizungumza kwenye Show ya SalamaNa inayoruka kila siku ya Alhamisi saa 3:00 usiku kupitia East Africa TV, Sebastian Ndege amesema kuna hisia tatu ambazo watu walikuwa na mashaka naye wakati anamchukua Harmonize.

"Kuna hisia tatu ambazo watu walikuwa wana mashaka mimi kuwa meneja wa Harmonize, moja ni kumfelisha dogo, mbili ni kumpoteza tatu ni kumtoa WCB, lakini ukweli ni kwamba mimi nilisubiri muda wake uishe ili niweze kufanya naye kazi" amesema Meneja wa Harmonize Dr Sebastian Ndege