Jumatatu , 10th Oct , 2022

Rapa wa Majengo Sokoni Music Moni Centrozone amesema hakuna msanii asiyetaka kufanya kazi na Mr Blue kwa sababu ameshawishi wasanii wengi kuamini kutoka sio lazima uwe na umri mkubwa.

Picha ya Moni Centrozone na Mr Blue kulia.

"Kila mtu anataka kufanya wimbo na Mr Blue, ndio amefanya sisi tuamini wakati tupo wadogo kwamba msanii kutoka sio lazima uwe na mkubwa, ameinspire wengi tulivyokuwa watoto kufanya mziki" - amesema Moni Centrozone 

Moni ameongeza kusema ikitokea anafanya kazi na Mr Blue ataenda na Producer S2Kizzy mpaka nyumbani kwa Blue Tabata kurekodi.