.Tunda na mpenzi wake mpya
Kupitia katika mtandao wa Instagram, ukurasa wa Tunda amepost picha ya mpenzi wake mpya aitwaye Otike raia wa Nigeria, ambaye anasadikika kuwa naye kwenye mahusiano kwa sasa kisha akaweka alama ya kopa na kuandika "Povu ruksa".
Baada ya muda mfupi Tunda kupost picha hiyo Otike mwenyewe alikuja ku-comment kwenye picha hiyo kwa kuandika "Nakupenda my Princess".
Penzi la Tunda na Whozu limedumu kwa muda wa mwaka mmoja, na katika historia inaonyesha Whozu ndiyo mwanaume ambaye ameweza kukaa na Tunda kwa muda mrefu zaidi kwenye mahusiano.